.
28th December, 2017
Hospitali ya kimishenari ya St Mary’s katika eneo bunge la Langáta jijini Nairobi liligeuka eneo la kupimana nguvu baina ya usimamizi wa kale na usimamizi mpya uliofika kutekeleza ilani ya mahakama ya kutaka usimamizi wa zamani uondoke. Baadhi ya matabibu walifurushwa huku wagonjwa wakisalia bila matibabu yoyote. Willy Lusige anaarifu. Ndivyo mambo yalivyokuwa katika hospitali ya St Mary, katika eneo la Langáta. Usimamizi mpya uliingia kwa vishindo na wafanyikazi wapya. Nao wafanyikazi wa kale waliojaribu kuzuia ujio huo mpya wakifahamu maana ya methali mwenye nguvu mpishe.