.
6th December, 2016
Kinara wa CORD Raila Odinga amesema yuko tayari kuungana na kinara wa ANC Musalia Mudavadi ili kuibandua serikali ya Jubilee. Viongozi hao walijumuika katika kaunti ya Laikipia wakitangaza kujuta kutengana kwenye uchaguzi mkuu uliopita. Haya yanajiri huku rais Kenyatta na naibu wake wakikita kambi katika ngome ya kisiasa eneo la mashariki ngome ya kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka.