.
5th December, 2016
Katibu mkuu wa vyama vya wafanyikazi nchini Francis Atwoli amekosoa serikali ya Jubilee kwa mgomo wa kitaifa wa madaktari na wauguzi. Atwoli amemlaumu rais kenyatta na serikali yake kwa kutozingatia majadiliano ya kukomesha mgomo kwa wakati uliofaa jinsi walivyokuwa wakifanya watangulizi wao marais wastaafu Mwai Kibaki na Daniel Toroitich Arap Moi. Atwoli alisema hayo alipokuwa akizungumza na wazee wajamii ya Waluhya kutoka Busia.