28th November, 2016
Mwanahabari wa KTN News Joy Doreen Biira ameachilia na maafisa polisi nchini Uganda lakini atafunguliwa mashataka ya ugaidi. Kesi ya Joy itasikizwa tarehe saba Disemba. Joy alikamatwa na mfalme wa Rwenzururu magharibi mwa Uganda baada ya makabiliano kuzuka katika ya maafisa wa polisi na walinzi wa mfalme huyo. Msemaji wa polisi Felix Kaweesi amesema kuwa joy alikamatwa baada ya kutuma picha za mapigano katika mitandao kinyume cha sharia.