28th November, 2016
Gavana wa Kilifi Amason Jeffa Kingi leo alifika katika tume ya maadili inayopambana na ufisadi EACC baada ya kuagizwa kufanya hivyo. Kingi ambaye aliandamana na wanasiasa mbalimbali aliwasili katika EACC na kuchukua muda mrefu kusema anayojua kuhusu ufisadi wa shilingi milioni 51 unaodaiwa kufanyika katika kaunti yake. Baadhi ya wanasiasa wamemtaka Kingi ajiuzulu kutokana na madai kuwa kaunti yake inakabiliwa na ufisadi mkubwa