28th November, 2016
Aliyekuwa naibu mkurugenzi wa NYS Harakhe Adan na aliyekuwa afisa katika wizara ya ugatuzi Hassan Noor wamekanusha mashtaka yanayowakabili ya kutoa zabuni za NYS kinyume na sheria walipokuwa afisini. Wawili hao walikuwa waliachiliwa mahakamani kwa dhamana ya shilingi milioni moja baada ya kukanusha mashtaka yaliyowasilishwa dhidi yao na tume ya kupambana na ufisadi nchini EACC. Harakhe ametajwa na mashahidi wengi kuwa alichangia kwa njia moja au nyingine kupotea kwa mamilioni fedha za NYS. Mahakama ilikuwa imetoa kibali cha kumkamata Harakhe baada ya kuonekana kutoshirikiana na vyombo vilivyokuwa vikichunguza sakata ya NYS