.
24th November, 2016
Maandamano yalishuhudiwa nje ya afisi ya Gavana wa Kilifi Amason Kingi baada ya mvutano wa makundi mawili kujiri. Mvutano huu ulioshuhdiwa kwa takriban saa nne ulisistisha shughuli za usafiri na uchukuzi katika mji wa Kilifi, kundi moja lilokuwa likimshikiniza gavana wa Kilifi kujiondoa lilianza msafara wake wa maandamano katika eneo la Kibaoni hadi katika afisi za gavana pale ambapo walikumbana na kundi jingine lilomtaka Uhuru na Ruto kujiondoa na hapo mtafuruku ukaanza na kuwabidi maafisa wa polisi kuingilia kati. Biashara na shughuli zilizistishwa huku maafisa wa usalama wakijaribu kusistisha mvutano huo.