.
22nd November, 2016
Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga amesema kuwa chama chake tayari kimepiga hatua kwa msajili wa vyama vya siasa kikitaka viongozi walioasi kupokonywa nafasi zao za uongozi. Wakati huo huo Raila ameilaumu serikali kwa kile anachokidai kwamba serikali ya Jubilee imewapuuza wananchi wanaoishi na ulemavu mbalimbali. Raila aliyasema hayo mapema leo katika jumba la Orange house hapa Nairobi, alipokutana na kikundi cha wananchi wanaoishi na ulemavu.