.
8th November, 2016
Waziri wa Afya Cleopa Mailu mapema hii leo alifika katika kamati ya seneti kuhusu afya kuhojiwa kuhusu madai ya ubadhirifu wa fedha takriban billioni tano katika wizara hiyo, waziri huyo alijitetea kuhusu madai hayo huku mwenyekiti wa kamati hiyo Wilfred Machage akimhoji kuhusu madai ufujaji wa fedha hizo. Wiki iliyopita waziri mailu alifika katika afisi za tume ya kupambana na ufisadi, EACC kujibu tuhuma hizo za ubadhirifu wa fedha.