.
3rd November, 2016
Polisi huko Kajiado wanamsaka mshukiwa mmoja aliyejaribu kumhonga naibu kamishina wa kaunti hiyo Alex Mutua juu ya uchunguzi unaoendelea kuhusu shamba la Mailwa. Kwa mujibu wa Mutua, mshukiwa huyo aliingia ofisini mwake na kudondosha kitita cha noti na kuondoka. Kamishina wa kaunti hiyo Harsama Kello amefafanua kwamba kinyume cha ilivyoripotiwa kwenye vyombo vya habari, Alex Mutua hakukamatwa na maafisa wa EACC.