3rd November, 2016
Rais Uhuru Kenyatta amesimama na uamuzi wa Kenya kukiondoa kikosi cha wanajeshi wake nchini Sudan kusini kinachohudumu chini ya umoja wa mataifa yaani South Sudan peace mission in South Sudan. Akizungumza katika hafla ya kufuzu kwa kikosi cha maafisa wa kadeti katika taasisi ya Kenya military academy huko Lanet katika kaunti ya Nakuru rais Uhuru alielezea kugadhabishwa kwake na hatua ya umoja wa mataifa ya kumfuta kazi luteni jenerali Johnson Kimani Ondieki kwa madai ya kufeli katika oparesheni ya kuwalinda raia wa Sudan kusini katika gasia za mwezi Januari mjini juba.uhuru aidha aliviomba vikosi vya kadet kuwa msitari wa mbele katika kuilinda Kenya bila kuisaliti amani ya nchi hii. Tangazo la kumfuta kazi luteni jenerali Johnson lilitolewa na katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki Moon mnamo jumamosi wiki hii na kufuatiwa na amri ya kuondoa kikosi cha Kenya nchini Sudan kusini hapo jana.