2nd November, 2016
Wakimbizi wa ndani waliokuwa wamekita kambi nje ya bunge walisafirishwa hadi Nakuru jana usiku baada ya kuishi maeneo ya bunge kwa takriban mwezi mmoja. Wakimbizi hao wamelalamikia kudhulumiwa na polisi kwa kupigwa wakati walipolazimishwa kupanda malori yaliyowasafirisha hadi Nakuru. Aidha wameilaumu serikali kwa kutotimiza ahadi walizopewa wakati walipokuwa nje ya bunge. Ombi lao ni kuwa rais Uhuru Kenyatta atawapa makao mbadala baada ya kuishi Uganda kwa muda mrefu tangu 2008 ambapo walitoroka ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa 2007.