.
31st October, 2016
Wanafunzi wa shule mbalimbali za msingi leo walikuwa kwa matayarisho ya kufanya mtihani wa kitaifa wa shule za msingi unaoanza hapo kesho kote nchini. Mtihani huu unaanza wakati wizara ya elimu imeshirikiana na ile ya usalama wa kitaifa pamoja na ya mawasiliano kuhakikisha wizi wa mitihani unathibitiwa mwaka huu. Moja ya masharti yaliyoweka na wizara ya elimu yanajumusha walimu wote kuwa shuleni wakati inapofanywa mitihani hii ambao inakamilika alhamisi wiki hii.