22nd October, 2016
Zaidi ya wafungwa 200 wa gereza la Nakuru mapema hii leo waliachiliwa huru. Hatua hiyo ni kufuatia agizo la rais kuwaachilia zaidi ya wafungwa elfu saba. Miongoni mwa walioachiliwa ni Robert Malakwen kutoka Salgaa eneo bunge la Rongai aliyehukumu kifungo cha miaka minane.