.
6th October, 2016
Kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga amesisitiza kuwa ni sharti Kenya itekeleze ripoti ya tume ya ukweli, haki na maridhiano, TJRC ili kutatua dhana ya maeneo fulani kuhisi kutengwa. Raila alikuwa akizungumza huko Kilifi alipokuwa mgeni wa heshima kwenye kongamano la uwekezaji liliondaliwa na serikali ya kaunti hiyo.