.
5th October, 2016
Wanafunzi wa chuo kikuu cha Eldoret walizua kizaazaa adhuhuri ya leo na kuwapa polisi wakati mgumu walipoandamana wakitaka kurejeshwa kwa aliyekuwa kiongozi wa taasisi hio Edgar Kisanya. Inaripotiwa kuwa Kisanya aliyetimuliwa chuoni humo alifanya jaribio la kutaka kujitoa uhai kwa kunywa sumu, kutokana na uamuzi wa mamlaka ya chuo hicho. Wanafunzi wanadai kuwa alitimuliwa chuoni humo bila makosa.