.
4th October, 2016
Gavana wa Meru Peter Munya mapema leo alifika mbele ya kamati ya uhasibu na uwekezaji katika bunge la seneti ili kutoa mwanga kwa tuhuma za kukosa kutoa hesabu ya fedha zilizotumika katika mwaka 2013/2014. Kwa mujibu wa mkaguzi wa fedha, mawaziri wa kaunti hawakutoa ripoti ya jinsi milioni 26.3 zilivyotumika kwenye ununuzi wa huduma na bidhaa.