.
2nd October, 2016
Mzozo wa ubabe umeibuka upya kati ya gavana wa Mombasa Ali Hassan Joho na mkuu wa kanda ya Pwani Nelson Marwa kuhusu ardhi. Marwa ametishia kumkamata Joho kuhusu ardhi inayopatikana Bombolulu ambayo inang’ang’aniwa na serikali ya kaunti na shirika la KBC. Wiki iliyopita vijana waliangusha ua katika ardhi hiyo ya ekari 22 kwa uelekezi wa gavana Ali Hassan Joho