.
29th September, 2016
Kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga hivi leo alikuwa maeneo ya Narok kunadi sera na kampeini za chama hicho na mrengo mzima wa CORD, kwenye msururu wa kampeini zake nchini. Wakati huohuo gavana wa Kisumu Jack Ranguma na mwenyekiti wa ODM kaunti ya Kisumu Prof Ayiecho Olweny wamewaeleza wanahabari jioni kuhusu maandalizi ya mkutano wa hadhara utakaoongozwa na Raila Odinga mjini Kisumu mwishoni mwa juma hili.