.
27th September, 2016
Kutoka Kisumu, polisi wanasubiri uchunguzi wa maiti kubainisha kiini cha kifo cha mwanamke mmoja katika kijiji cha Kombewa kwenye kaunti ya Kisumu. Emelda Atieno naibu mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Nyalik alifariki hospitalini siku ya Jumapili. Kifo chake kimezua utata huku familia ikidai kwamba alifariki kutokana na kichapo kutoka kwa mumewe huku naibu chifu wa eneo hilo akidai kwa upande mwingine kuwa mwendazake alikunywa sumu usiku baada ya kuzozozana na mumewe ambaye anazuiliwa na polisi kwa sasa kusububiri uchunguzi