.
20th September, 2016
Matatizo ya kifedha yanakumba kamati aandalizi ya mashindano ya dunia ya riadha ya wanariadha wasiozidi umri wa miaka kumi na minane. Kenya iliteuliwa kuwa mwenyeji wa mashindano hayo miaka miwili iliyopita baada ya Jiji la Nairobi kupitia shirikisho la riadha kuweka wazi nia ya kutaka kuwakaribisha wanariadha chipukizi hapa nchini. Hata hivyo kufikia sasa kamati andalizi haijaanza maandalizi rasmi kwani wizara ya michezo bado haijatenga fedha zinazohitajika.