13th September, 2016
Hakuna apendaye kujihusisha na mauti, pamoja na kwamba kila nafsi itaonja mauti jinsi ilivyoandikwa kwenye vitabu vitakatifu. Huko Eldoret eneo la Teleview, wenyeji wamepinga kujengwa kwa hifadhi ya maiti katika eneo lao, wakisema si vyema kuishi karibu na maiti.