×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Waumini wa dini ya Kiislamu waadhinisha sikukuu ya Idd-ul-Adha

12th September, 2016

Maelfu ya waumini wa dini ya kiislamu leo wamekongamana katika misikiti na viwanja mbalimbali kwa sala ya kuadhimisha sikukuu ya Idd-ul-Adha sikukuu hii hufahamika zaidi kama idd ya kuchinja ambapo waumini hukumbuka jinsi Abrahamu alivyowekwa kwenye majaribu ya kumtii mungu kwa vyovyote. Alitakiwa kumtoa mwanawe wa kiume kama sadaka lakini mungu akampa kondoo alipoonesha nia ya kumtii. Katika kaunti ya Isiolo, viongozi wa dini waliwarai waumini waliohudhuria sala hiyo katika uwanja wa kaunti ya Isiolo kudumisha amani.  Kule Mombasa sala ya kuadhimisha sikukuu ya Idd ilifanyika katika shule ya msingi ya Ronald Ngala.  Viongozi waliohudhuria hafla hiyo wamesisitizia umuhimu wa amani na utangamano nchini. Isitoshe wamekashifu shambulizi la jana ambapo kituo cha polisi kilivamiwa na kundi la wanawake waliokuwa na bomu la petroli na silaha nyengine.

.
RELATED VIDEOS