Ekuru Aukot aitetea IEBC
6th August, 2016
Kiongozi wa chama cha Third Way Alliance Party, Dkt Ekuru Aukot amekosoa maafikiano ya kuwaondoa afisini makamishna wa IEBC. Aukot amefananisha hatua hiyo na mbinu ya wanasiasa kujinufaisha kutokana na masaibu ya Wakenya. Aidha, aukot amepuuzilia mbali matokeo ya kura za maoni, akisema mara nyingi zinatumika kuondoa fikira za wakenya kutoka kwenye masuala yenye umuhimu kwao, alizungumza pamoja na maafisa wa chama chake kwenye afisi zao hapa jijini Nairobi.