Mbio za Mwea Classic yamezinduliwa leo yakinuiwa kuwavutia zaidi ya wanariadha 1500
4th August, 2016
Makala ya saba ya mbio za Mwea Classic yamezinduliwa leo katika hoteli moja mjini Nairobi yakinuiwa kuwavutia zaidi ya wanariadha 1500. Mbio hizo ambazo zilianzishwa mnamo mwaka 2009 kwa lengo la kuboresha viwango vya elimu katika eneo la Mwea zitaandaliwa tarehe 17 mwezi Septemba katika uwanja wa Wang’uru. Makala ya mwaka huu yatakuwa na vitengo vitatu ambavyo ni mbio za kilomita 5, mbio za kilomita 10 na nusu marathon. Washindi watatunukiwa medali na pesa. Tangu kuasisiwa kwake, mashindano hayo yametoa wanariadha mahiri nchini kama vile Hellen Obiri.