Kituo cha polisi walikokuwa wamefungiwa marehemu Willie Kimani na wenzake kiliteketezwa
6th July, 2016
Mapema leo kituo cha polisi walikokuwa wamefungiwa kinyume cha sheria marehemu wakili Willie Kimani, mteja wake na dereva wa teksi kiliteketezwa. Watatu hao walifungiwa katika kituo cha Syokimau kabla ya kuuawa. Wakati huohuo mwanapatholojia wa chama cha wanasheria nchini LSK, ameieleza mahakam kuwa watatu hao hawangeweza kustahimili uchungu mwingi uliotokana na mateso ikiwemo kufinywa sehemu zao za siri. Nicholas Wambua amekuwa akifuatilia taarifa hiyo na hii hapa taarifa yake.