Waziri wa Elimu Fred Matiang’i amewatahadharisha wanafunzi wanaojihusisha na vitendo vya kihuni
27th June, 2016
Waziri wa Elimu Fred Matiang’i amewatahadharisha wanafunzi wanaojihusisha na vitendo vya kihuni shuleni akisema watawajibikia uharibifu wanaofanya. Akizungumza kuhusu tukio la wanafunzi kuteketeza mabweni 7 katika shule ya upili ya Itiero. Matiang’i amesema wanafunzi waliohusika watahitaji idhini kutoka kwa wizara ikiwa watataka kuhamia shule nyingine. Aidha amesema serikali haitagharamia uharibifu huo