Francis Ole Kaparo na kundi lake wamezuiwa kuhutubia kwenye mpaka kati ya Kaunti za Kisumu na Nandi
22nd June, 2016
Mwenyekiti wa Tume ya Haki na Maridhiano Francis Ole Kaparo na kundi lake leo wamezuiwa kuhutubia wakazi waliokuwa na ghadhabu katika vituo vya biashara vya Songor na Kopere kwenye mpaka kati ya Kaunti za Kisumu na Nandi. Kaparo na kundi lake walikuwa wameenda kwa mkutano wa kurejesha amani kufuatia mapigano ya siku mbili katika eneo hilo ambayo yamesababisha vifo vya watu wawaili na zaidi ya watano kujeruhiwa. Rashid Ronald alikuwepo na ametuandalia taarifa ifuatayo.