Shofco yahubiri Amani kwa wakaazi wa Kibra
18th June, 2016
Wakaazi wa Kibra mapema leo wamejitenga na dhana kwamba mtaa huo ni mahali pa fujo na maandamano. Wakaazi, walitangamana na shirika moja linalotambulika katika mitaa ya mabanda ya Kibra na Mathare kama shining hope for communities, kuhubiri amani. Hafla hiyo ilijumuisha michezo mbalimbali kama ndondi na kadhalika waandalizi wa shughuli hiyo wakiongozwa afisa mkuu mtendaji wa Shofco walisema kuwa vijana wa Kibra hawatakiwi kutumiwa visivyo na wanasiasa.