Mwanamke mwenye asili ya Brazil ameishi nchini kwa zaidi ya miaka 40
5th June, 2016
Mwanamke mmoja mwenye asili ya Brazil ameishi humu nchini kwa zaidi ya miaka 40 katika eneo la likuyani kaunti ya kakamega. Elvis kosgei alimtembelea mwanamke huyu nyumbani kwake kongoni ambapo anaishi tu kwa amri ya mungu kutokana na mazingira alimokuwa. Mbali na hayo amedai kujaribu kutafuta usaidizi kutoka kwa balozi ya brazil bila mafanikio yoyote.