Wanafunzi 5 wa shule ya Mwariki Nakuru wadai kufukuzwa shuleni kwa kutohudhuria masomo ya ziada
9th June, 2015
Wanafunzi watano wa shule ya upili ya Mwariki kaunti ya Nakuru wamelazimika kusomea nyumbani, wakidai kuwa walifukuzwa shuleni baada ya kukosa kuhudhuria masomo ya ziada siku ya Jumamosi. Kulingana na wanafunzi hao na wazazi wao mwalimu mkuu aliwafukuza na kuashiria kuwa hatowaruhusu tena katika shule hiyo.