.
21st February, 2022
Mwanaharakati wa kisiasa Stanley Livondo leo alifika katika makao makuu ya upelelezi wa makosa ya jinai DCI, kuandikisha taarifa kuhusu matamshi aliyotoa jumamosi iliyopita, akidai kwamba kulikuwa na njama ya kumdhuru rais Uhuru Kenyatta miaka kadhaa iliyopita njama ambayo alidai ilipangwa na naibu rais William Ruto. Livondo, aliyeandamana na wakili wake, alisema bado anashikilia madai yake, akiongeza kwamba amewakabidhi wapelelezi wa DCI taarifa nyeti kuhusu swala hilo. Na kama anavyoarifu mwanahabari wetu Emmanuel Too, Livondo aliachiliwa huru baada ya kuandikisha taarifa hiyo.