.
21st February, 2022
Muungano wa kisiasa wa Azimio la Umoja umeendeleza kampeni zake katika maeneo mbali mbali nchini, katika eneo la Magharibi muungano huo umeandaa mkutano mkubwa katika kaunti ya Vihiga. Kinara wa ODM Raila Odinga amewaongoza wafuasi wake katika muungano huo kuuza sera zake katika eneo la Pwani na kuwaahidi mabadiliko makubwa ikiwemo kuiboresha bandari ya Shimoni endapo atachaguliwa.