.
21st February, 2022
Muungano wa Kenya kwanza sasa unaishutumu serikali kutokana na kile wanachokitaja kama kuwapuuza wakenya gharama ya maisha ikizidi kupanda kila uchao. Wakizungumza na wanahabari na kisha baadaye kwenye mikutano ya hadhara katika kaunti ya Meru wanasiasa hao wamemshutumu waziri wa fedha Ukur Yattani wakidai alipitisha kiwango kinachokubaliwa kisheria kukopa pesa bila ya idhini ya bunge.