.
26th January, 2022
Gavana wa kaunti ya Kitui Charity Ngilu ameimarisha wito wake wa kumtaka kiongozi wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka kujiunga na vuguvugu la Azimio la Umoja na kuunga mkono azma ya Raila Odinga kugombea kiti cha urais.
Akizungumza katika mkutano wa wajumbe kutoka maeneo mbali mbali ya kaunti ya Kitui, Ngilu amesema kuwa dalili zote sasa zinaonyesha kuwa Kalonzo anastahili kujiunga na Azimio la Umoja na kuweka mkataba wa kubuni serikali ijayo na kiongozi wa ODM Raila Odinga.