26th January, 2022
Muungano wa One Kenya Alliance umeanza juhudi zakutafuta uungwaji mkono kutoka kwa wanasiasa wengine baada ya kinara wa ANC Musalia Mudavadi na Moses Wetangula wa Ford Kenya kutorokea mrengo wa Naib Rais William Ruto.
Kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka amefanya mkutano na mfanyabiashara Jimi Wanjigi, katika kile kinachokisiwa kuwa ni kupanga mikakati ya muungano wa kiasa kuimarisha OKA inayomshirikisha pia mwenyekiti wa KANU Gideon Moi.