.
15th January, 2022
Mkurugenzi wa mashtaka ya umma Noordin Hajji amempa siku thelathini inspekta mkuu wa polisi Hillary Mutyambai kuanzisha uchunguzi na kupeana majibu ya uchunguzi huo kuhusiana na ukurasa mmoja wa facebook unaotuhumiwa kutumiwa kwa uchochezi katika kaunti ya Lamu. Hili linajiri wakati serikali imeanza kuwasaka wachochezi na magaidi wa Al Shabaab waliohusika na mauaji ya zaidi watu kumi na tatu wakiwemo maafisa wanne wa polisi chini ya siku kumi zilizopita.