.
14th January, 2022
Wafuasi wa muungano wa One Kenya Alliance wataendelea kusubiri kabla ya kutangazwa kwa kinara atakayepeperusha bendera ya muungano huo katika uchaguzi mkuu ujao. Kulingana na mwenyekiti wa kamati ya ufundi ya muungano huo Sammy Karanja, tayari ripoti ya jinsi atakavyochaguliwa mgombea wa urais ipo tayari na kinacho subiriwa ni kujulishwa na kukubaliana na wajumbe wa vyama tanzu kabla ya tangazo hilo kufanywa. Wakati uo huo, vinara wa One Kenya wamekanusha madai ya kuibuka kwa mianya katika muungano wao na kuwa Musalia Mudavadi yumo katika safari ya kugura OKA.