.
14th January, 2022
Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga leo hii hii ametua na msafara wa azimio la umoja katika kaunti ya Taita Taveta ambapo amefaulu kuwavutia upande wake wanasiasa kutoka vyama pinzani na wakati uo huo kuwaonya wapiga kura dhidi ya kumchagua naibu rais William Ruto. Gavana wa kaunti ya Taita Taveta Granton Samboja aliechaguliwa kupitia chama cha wiper na mbunge wa Taveta Naomi Shaaban wa Jubilee wote wakionyesha imani ya Odinga kuwa rais wa tano.