.
5th December, 2021
Naibu Rais William Ruto ameendeleza kampeni yake kwa siku ya pili mfululizo katika kaunti ya Nyeri kwa kuhudhuria ibaada ya jumapili makanisa ya eneo bunge la Tetu. Baadhi ya viongozi wa kisiasa kutoka eneo hilo walitangaza rasmi kugura chama cha jubilee na kujiunga na chama chake cha UDA. Miongoni mwa viongozi waliojiunga na UDA ni mbunge wa Tetu Gichuhi Mwangi na Gavana wa Nyeri Mutahi Kahiga aliyesema kwamba wakati umewadia wa kufanya uamuzi kulingana na matakwa ya wapiga kura katika eneo hilo.