.
5th December, 2021
Shughuli ya kuwaokoa wachimba migodi kwenye mgodi wa Abimbo kule Bondo, kaunti ya Siaya bado inaendelea. kufikia sasa, ni wachimba migodi watatu ambao wameokolewa, huku mmoja akipatikana akiwa ameaga dunia. Shughuli ya kuwaokoa ikiendelea, kati ya watu nane waliofunikwa katika mgodi huo siku nne zilizopita, wanne bado hawajapatikana. Michael Onyango ambaye aliokolewa jana usiku, na Bernard Ochieng aliyeiokolewa leo asubuhi. Wanaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya bondo.