25th October, 2021
Waziri wa usalama wa ndani Fred Matiang’i sasa amedokeza kuwa wanawasilisha ombi rasmi kwa tume ya uchaguzi IEBC kuwazuia wanasiasa wote wanaojihusisha na ghasia na vurugu kwenye kampeni zao. Waziri Matiang’i anasema idara za usalama zinaushahidi wa kutosha kuhusu baadhi ya wanasiasa wanaoendeleza uchochezi kwenye uchaguzi mkuu ujao. Matiangi alizungumza kwenye warsha kuhusu maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao iliyojumuiasha taasisi mbalimbali za serikali zikiwemo IEBC na mahakama.