.
25th October, 2021
Kiongozi wa chama cha Odm Raila Odinga amekariri msimamo wake wa kuwapa vijana wasiokuwa na kazi shilingi elfu sita kila mwezi wa kujikimu kimaisha. Akizungumza mjini kisumu katika ziara ya kuhamasiha umma kujiandikisha kama wapiga kura, Odinga alisemawale wanaomkejeli wanakosea, kwani akiwa waziri mkuu, aliona mianya iliyokuwa ikipoteza pesa za umma na kwa hivyo ana hakika kuwa atatimiza ahadi yake.