.
20th October, 2021
Wakenya waliochukua mikopo isiyozidi shilingi milioni 5 kuanzia mwezi oktoba mwaka jana na kushindwa kuilipa kwa wakati wamepata afueni baada ya Rais Uhuru Kenyatta kuzitaka mamlaka zinazohusika kutowa orodhesha kuwa miongoni mwa walioshindwa kuilipa na shirika la kufuatilia wasiolipa mikopo CRB kwa muda wa miezi kumi na miwili ijayo. Vile vile akielezea wasiwasi kuwa juhudi zilizofanywa kuimarisha uchumi huenda zikadidimia kutokana na ongezeko la bei ya mafuta nchini.