.
20th October, 2021
Majonzi yalitanda katika kijiji cha miti mingi huko Elementaita eneo bunge la Gilgil baada ya mwanamume wa miaka 49 kudaiwa kumuua msichana wa miaka 16 aliyekuwa mwanafunzi wa kidato cha tatu kwa kumdunga kisu kabla ya kujitia kitanzi. Inadaiwa kuwa Salim said, alimuua Naomi Nyarangi mapema leo hii kiini cha mauaji hayo kikiwa hakijulikani. Salim baadaye alijitia kitanzi huku duru zikiarifu kuwa wawili hao walikuwa na uhusiano wa kimapenzi kabla ya kisa hicho.