13th October, 2021
Baadhi ya mataifa yametupilia mbali sheria zinazoangazia kujitoa uhai kama kosa la jinai. Hii ni mojawapo ya njia ya kupunguza visa hivyo kama njia ya kuwahimiza waathiriwa kutafuta matibabu. Hata hivyo barani Afrika haswa Kenya, swala hili ni zito kwa wale wanaopatikana na hatia ya kutaka kujitoa uhai. Mwanahabari wetu Saada Hassan analivalia njuga swala hili katika msururu wa Makala maalum ya Akili ni Afya.