.
2nd August, 2021
Zaidi ya wanafunzi milioni moja waliokamilisha elimu ya shule ya msingi wameanza safari yao ya elimu ya sekondari kwa kujiunga na kidato cha kwanza hivi leo. Kwa wengi muhula wa kwanza uliwaanzia vizuri baada ya kupata nafasi lakini kwa baadhi mambo hayakuwa mazuri baada ya kunyimwa nafasi ya kuingia shuleni kutokana na sababu mbali mbali. Kulingana na mwenyekiti wa muungano wa wazazi nchini pta nicholas maiyo, wazazi wengi walilazimishwa kununua sare za shule kutoka kwenye maduka yaliyoidhinishwa nashule husika, baadhi ya wanafunzi wakinyimwa fursa kwa sababu ya alama walizopata katika mtihani wa kitaifa.