1st August, 2021
Kwenye maswala ya afya mwaka wa 2018 utakumbuka kwamba Rais Uhuru Kenyatta alitangaza mpango wa afya bora na nafuu kwa wote yaani Universal Health Coverage kama mojawapo ya ajenda zake nne kuu ? mpango ambao ulinuia kuhakikisha kwamba wakenya wanapokea matibabu ya hali ya juu na kwa bei nafuu kabla ya mwaka 2022. Miezi michache tu imesalia kabla ya mwaka 2022 kuwadia, je, hali iko vipi tangu jaribio la mpango huo katika kaunti nne za Isiolo, Nyeri, Machakos na Kisumu?