1st August, 2021
Seneta wa Baringo na mwenyekiti wa chama cha Kanu Gideon Moi, amewaonya vikali maafisa katika wizara ya maji kuhusiana na kukwama kwa awamu ya pili ya ujenzi wa bwawa la Kirandich lililoko eneo la Kabarnet. Moi aliyekuwa akizungumza katika kanisa la AIC kabarnet, amesema kuwa mradi huo ulioratibiwa kugharimu shilingi bilioni 2, ulikuwa unalenga kuwanufaisha wakazi wa eneo hilo. Amezitaka idara husika, kuwachukulia hatua kali wote waliohusika katika ubadhirifu wa fedha zilizokusudiwa mradi huo.