1st August, 2021
Kiongozi wa chama cha Odm Raila Odinga amesema chama chake kitaunda miungano na vyama vingine vya kisiasa vyenye falsafa sawa na ya Odm baada ya kukutana na waakilishi wa chama hicho kote nchini. Akizungumza hii leo katika kaunti ya Vihiga, Odinga amesema wakati umewadia wa kutembea njia mbadala ya kisiasa baada ya muungano wa Nasa kusambaratika. Kwa upande wake Naibu Rais William Ruto aliendelea kutetea mfumo wake wa kiuchumi wa Bottoms Up ambao umekejeliwa na wapinzani wake akisema unalenga kuwainua kiuchumi walala hoi.